Sunday, May 10, 2020

MJASIRIAMALI : KUWA KING"ANG"ANIZI UTAFANIKIWA SANA

Kuendelea kung’ang’ania na kutaka matokeo unayataka yatokee kwenye maisha yako, naweza kusema hili ni moja ya jambo la muhimu sana katika ujasiriamali. Iko wazi utakutana na changamoto kwenye njia ya mafanikio, lakini huwezi kuchoka ni lazima ung’ang’anie mpaka lile lengo lako liweze kutimia.
Unapokutana na changamoto na ukaamua kuwa mbishi kwa kupambana nazo, hapo utakuwa upo kwenye njia sahihi ya mafanikio yako. Wajasiramali walio wengi ni watu wa kung’ang’ania na kwa sababu hiyo huwasaidia sana kuweza kufikia mafanikio yako. Ukishindwa kuwa king’ang’anizi sahau mafanikio ya ujasiriamali.

No comments:

Post a Comment